Thursday 4 October 2012

Dr Slaa kutikisa Arusha Siku ya Jumamosi

 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) anatarajiwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika jiji la Arusha siku ya Jumamosi tarehe 06.10.2012 kuanzia saa 8 mchana. Pamoja na mambo mengine Kiongozi huyo wa CDM pia atatumia mkutano huo kuzindua rasmi kampeni za udiwani katika kata ya daraja mbili,uzinduzi huo utafanyika katika viwanja vilivyopo mtaa wa NDARVOI.

Tayari kuna hekaheka kubwa katika jiji la Arusha kuhusiana na mkutano huo ambapo mazungumzo ya watu mbalimbali yanazungumzia mkutano huo unaotarajiwa kuwa gumzo.

Taarifa za awali zinasema mkutano huo pia utatumika kufuta nyayo za chama cha CUF ambacho kilisomba watu Dar-es-Salaam kwenda kuwahutubia Arusha ili kuepuka aibu ya kukosa watu.Pia inadaiwa wananchi wa Arusha wamedhamiria kuonyesha dunia uungaji mkono wao kwa chama cha CDM.

No comments:

Post a Comment

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU