Showing posts with label HABARI. Show all posts
Showing posts with label HABARI. Show all posts

Sunday 2 September 2012

Mwandishi wa habari wa channel 10 afariki baada ya polisi kuingilia mkutano wa CHADEMA Iringa



Pichani Daud Mwangosi akiwa kazini muda mfupi kabla kufikwa na mauti yake.)

 



Mh. Mbowe: Sisi sote ni ndugu, vyama vya siasa visitugombanishe, tutangulize Utanzania wetu, watanzania walikuwepo kabla ya vyama vya siasa, Tanzania inachanga moto nyingi kuliko malumbano vya chama vya siasa


Video ya Mkutano wa M4C Reading ulioandaliwa na Chadema UK 26.08.2012


Matukio mbalimbali katika mkutano wa M4C Reading

Mwenyekiti Mh Likosi Akihutubia Mkutano
Katibu wa Chadema UK Kamanda Liberatus Musiba akiwa na Mwenyekiti wakifuatilia mkutano
 
Mh Lukosi na Mweka Hazina Dr Alex  wakimsikiliza kwa makini Kamanda Godbless Lema akihutubia mkutano huo kwa njia ya simu
 
Dr Alex Paurine ambaye pia ni Mweka hazina akihutubia mkutano huo, Dr Paurine alitumia Power Point kuonyesha picha na matukio yanayoonyesha hali halisi ya maisha ya Watanzania wengi.
 
Ndg Aseri Katanga Mwenyekiti wa bodi ya Computer for Africa akihutubia

Mwenyekiti wa Baraza la wanawake Chadema UK Bi Jessica Maduhu akielezea masikitiko yake juu ya huduma mbovu za afya na kero wanazozipata wanawake wajawazito wakati wa kujifungua na huduma za afya kwa watoto.

Gerald Lusingu, Mmoja wa wenyeji wa Mkutano wa M4C Reading na aliyechaguliwa kuwa mwakilishi wa M4C Reading akiwasalimia wananchi 

Dr Lusingu akitoa Historia ya Harakati za Mabadiliko na Mageuzi katika nchi yetu, huku akifuatiliwa kwa makini na Katibu wa wanawake Bi Margaret Malekia, Katibu Mh Liberatus na Mwenyekiti Mh Lukosi 
Engineer Prudence Kahatano akichambua matokeo ya azimio la Zanzibar lililovunja azimio la Arusha na madhara ya soko huria kwa Watanzania
 

 Wadau Mbalimbali katika Mkutano

 


 Wanachama mbali mbali wakikabidhiwa kadi za Chadema na Mwenyekiti wa Chadema UK Mh Chriss Lukosi

Ndg Wambura akivalishwa Gwanda na Kupewa kadi ya Chadema na Mwenyekiti Mh Lukosi





Saturday 25 August 2012

TAARIFA YA USAFIRI KWENDA M4C READING

 TAWI LA CHADEMA UK LINAPENDA  KUWATANGAZIWA WANACHAMA WAKE WOTE, WATANZANIA WOTE NA WAPENZI WA CHADEMA WAISHIO LONDON KUWA  WAWASILIANE NA CHRIS LUKOSI KWA TARATIBU ZA USAFIRI WA KWENDA READING KUHUDHULIA MKUTANO WA M4C.

MAGARI YATAONDOKA SAA NNE ASUBUHI

Mkutano utafanyika siku ya Tarehe 26/08/2012 kuanzia saa saba mchana mpaka saa kumi na mbili jioni, siku ya Bank Holiday. Risc Reading International Solidarity Centre, 35-39 London Street, Reading, RG1 4PS .
 
WASOMI WENGI NA WANAHARAKATI MBALI MBALI WATAONGEA SIKU HIYO,
SIKU YA MKUTANO TUTAANZISHA MFUKO WA KUFA NA KUZIKANA KWA AJILI YA WATANZANIA WOTE WAISHIO UK BILA KUBAGUA CHAMA CHAKO CUF,CCM,UDP,TLP WOTE MNAKARIBISHWA
 
Watanzania wote na wadau mbali mbali mnakaribishwa
 
SISI SOTE NI NDUGU, TATIZO NI CCM
 
 ni wakati wa kusimama na kusema tumechoka
 
KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA HAWA WAFUATAO
MWENYEKITI: Chris Lukosi 07903828119
 
Au tutumie email kupitia chademauk@gmail.com
 
 
Peooooople's Power

Thursday 23 August 2012

Mwalimu mmoja wanafunzi 652

Akiwa katika Oparation Sangara inayoendelea hivi sasa nchini, Mwenyekiti wa Baraza la vijana la Chadema, Bwana Deogratias Munishi amegundua shule ambayo inawanafunzi 652 na Mwalimu mmoja tu. Shule hiyo ipo katika Kijiji cha Kadodo Kata ya  Luale, Mvomelo  Mkoani Morogoro.  Hii ndo hali halisi ya elimu Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru, chini ya utawala wa CCM. 
 
Mwenye shati la rangi ya udongo na suruali nyeusi ndiye Mwalimu Mkuu na Mwalimu pekee wa Shule ya Msingi Kododo iliyopo kata ya Luale, Mvomelo Mkoani Morogoro. Shule hiyo inawanafuzi 652.
 
 
Katibu Mkuu wa BAVICHA Deogratias Munishi akiwasikiliza kwa makini  Mwenyekiti wa kitongoji na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo walipo kuwa wakimuelezea hali halisi ya maendeleo ya elimu ya kijiji cha Kadodo
Katibu Mkuu wa BAVICHA Deogratias Munishi akimkabidhi kadi ya CHADEMA aliyekuwa mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Kododo jimbo la Mvomero, bwana Charles Kiwaga. Wengine ni wanachama wapya wa CHADEMA tawi la Kododo Mvomero.
 
Aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM kata ya Muhonda akieleza jinsi alivyokunwa na sera za CHADEMA zilizoelezwa na katibu Mkuu wa BAVICHA katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kichangani.

Tuesday 14 August 2012

CHADEMA KUWASHA MOTO KATIKA MJI WA READING SIKU YA TAREHE 26/08/2012

UK
Ili kufikia malengo yetu ya kuzunguka kwenye Miji mbalimbali ya UK kuhamasisha Watanzania waishio uk kujiunga na Chadema, kueneza kampeni ya m4c na  kufungua matawi mengine, Tawi la Chadema London linapenda kuwatangazia Watanzania wote waishio katika Mji wa Reading na maeneo ya jirani kuwa kutakuwa na mkutano mkubwa wa M4C UK utakao fanyika Tarehe 26/08/2012 siku ya Bank holiday.
Dhumuni  la mkutano huo ni kuwahamasisha Watanzania waishio UK kujiunga na chama, kushiriki katika harakati za mabadiliko, kusajili wanachama wapya, kuchagua  wawakilishi wa muda kutoka mji wa Reading pamoja na kuanzisha mfuko wa kufa na kuzikana kwa manufaa ya watanzania wote.
Tumekusudia kuanzisha Mfuko wa kufa na kuzikana kwa sababu mpaka hivi sasa Mtanzania akifariki akiwa  UK hakuna taasisi wala ofisi yoyote inayotoa msaada. Jukumu ambalo kwa muda mrefu Serikali yetu kupitia ubalozi umelipuuzia na kushindwa kulisimamia na kulishughulikia. 

Mfuko huu utasaidia katika kumsafirisha Marahemu na Mfiwa pamoja na kusaidia kushughulikia matatizo na usumbufu utakaojitokeza  baada ya mtu kufariki dunia na kusaidia matatizo mbalimbali yakiwemo majanga ya dharura.
Pia katika mkutano huo wanachama mbalimbali wa CCM walio na uchungu na nchi yetu na wanaopenda maendeleo na  mabadiliko ya kweli watapewa nafasi ya kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo kama sehemu moja wapo ya  kampeni yetu ya Kuvua Gamba na Kuvaa Gwanda ukiwa Ughaibuni.
Mkutano utafanyika siku ya Tarehe 26/08/2012, Kuanzia saa saba mchana mpaka saa kumi na mbii jioni.

Risc Reading International Solidarity Centre,
35-39 London Street,
Reading, RG1 4PS

 Watanzania wote, marafiki na wadau mbali mbali  wa maendeleo na mabadiliko ya kweli mnakaribishwa sana.  
Huu ndio wakati wa mabadiliko,  kusimama na kusema tumechoka!
KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA;

MWENYEKITI: Chris Lukosi 07903828119,
KATIBU MWENEZI:  Chris Chagula 07405889880
au
Tutumie email kupitia chademauk@gmail.com

HATULALI MPAKA KIELEWEKE!!!!!!!!!!!

Peooooople's Power




Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU