Sunday 30 December 2012

CHADEMA M4C-UK HATULALI MPAKA KIELEWEKE
                               
NDUGU MAKAMANDA!!!

NI BUSARA TUPONGEZANE NA KUMSHUKURU MUNGU KWA KUTUJALIA KUVUKA MWAKA 2012 NA KUANZA MWAKA 2013, TUKIWA NA HALI NZURI KIAFYA NA KTK HARAKATI ZA KUMKOMBOA MTANZANIA KIFIKRA.

TUNAJIVUNA KUMALIZA MWAKA KWA KISHINDO KWANI TUMEWEZA KUBAINI NA KUMWAJIBISHA VILIVYO KILA ALIYEFANYA KINYUME NA MATAKWA YA M4C NDANI YA CHADEMA KTK MAANDALIZI YA KUCHUKUA DOLA

NAFARIJIKA KUWAMBIA KWAMBA CHADEMA KUCHUKUA DOLA SI NDOTO TENA, BALI ITAKUWA. HIVYO TUNAWASHAULI KWA KUWAHIMIZA CCM WASIGHARIMIKE KWA KUTUMIA RASILIMALI ZETU NYINGI KUDHOOFISHA HARAKATI ZA UMMA WA WATANZANIA ZINAZOFANYIKA KUPITIA CHADEMA

NAPENDA NIWATIE MOYO KWAMBA, ZAIDI YA SISI (CHADEMA) KUTABILI USHINDI IFIKAPO MWAKA 2015, PIA UMMA TUNAOUPIGANIA UNAJITABILIA USHINDI MKUBWA DHIDI YA CCM LICHA YA PROPAGANDA CHAFU NA NJAMA NYINGINE POTOFU WANAZOZIFANYA KUPITIA VYOMBO VYA DOLA.

TUNAPENDA IELEWEKE KWAMBA MWAKA 2013 TUTAJIPANGA KAMA TAWI LA SERIKALI TARAJIWA YA CHADEMA. KWAHIYO, M4C-UK ITAKUWA KIMKAKATI ZAIDI KULIKO HAMASA. HIVYO TUMENUWIA KUWA NA VIONGOZI SAHIHI WENYE MAONO, WITO, FIKRA SAFI, UTU, NIDHAMU, NA NIA YA MAENDELEO MBADALA KWA WATANZANIA. KWA MANTIKI HII, TUNAKUOMBA WEWE BINAFSI UJIANDAE KUWANIA UONGOZI ILI UTULETEE NJOZI MPYA, ZITAKAZOTUVUSHA NGAMBO ILE  YENYE TANZANIA MPYA TUNAYOITAKA.

MWISHO WA YOTE NATUMIA FURSA HII KUTOA SHUKRANI ZA DHATI KWA UONGOZI WA MUDA NA BAADHI YENU MLIOJITOLEA KWA HALI NA MALI KUHAKIKISHA TAWI LETU LINASONGA MBELE. NAWATAKIA MWAKA MPYA WENYE MAFANIKIO MAKUBWA


MUNGU IBARIKI CHADEMA, MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE
Piipooooooooooz!!!!

IMETOLEWA NA KURUGENZI YA MWASILIANO NA MAHUSIANO YA CHADEMA-UK

Wednesday 12 December 2012


BREAKING NEWS!!!!!
Mwenyekiti wa CHADEMA UK Mr Christopher Lukosi amevuliwa madaraka na kusitishwa uanachama.
Ikiwa ni takribani miezi minne tangu tawi la CHADEMA UK lifunguliwe rasmi na Mr Godbless Lema, kumekuwepo na maendeleo makubwa ya ujenzi wa tawi hili lakini vile vile kumekuwepo na changa moto mbali mbali kutokana na uelewa wa watu ktk dhana nzima ya M4C. M4C ikiwa na maana ya Movement for Change, ni sharti mtu yeyote anayeingia ktk movement hii kwenye ngazi ya uongozi aelewe haya machache ya msingi:
1)   Kwanza aone matatizo yanayomgusa yeye na jamii yake
2)   Ajue na kutambua fika chimbuko la matatizo haya
3)   Awe tayari kuwa kiini cha mabadiliko ya kweli anayoyataka kwa jamii
4)   Aweze kutoa ufumbuzi kwa kukemea maovu, kuelimisha na hata yeye binafsi kuelimika
5)   Ili afanikiwe ktk kipengele cha (4) ni sharti ajitambue yeye binafsi ya kwamba ni:
i)            Lazima awe safi na mwenye sifa za kukemea waovu
ii)           Aweke maslahi ya jamii mbele na si yake binafsi
iii)         Awe na sifa za uongozi zinazotakiwa, nidhamu ikiwa nambari moja ktk orodha.
iv)         Awe na msimamo wa kiitikadi
Kwa hiyo, uongozi wa CHADEMA UK kwa baraka za watetezi wa haki ya kweli (CHADEMA TZ) unawatangazia umma watanzania kokote mlipo kwamba kuanzia leo tarehe 12/12/12, Mr Christopher Lukosi amevuliwa rasmi uongozi na amesitishwa uanachama kutokana na kutokidhi mengi ya yaliyotajwa hapo juu.
Uongozi wa CHADEMA UK unamshukuru sana kwa mchango na ushirikiano wake mkubwa kwa kipindi ambacho matundu ya chujio yalikuwa makubwa. Tutaendelea kumkumbuka na hata kutumia misemo yake yenye maana nzito kwa jamii ya kitanzania, kama vile: -
i)            Sisi sote ni ndugu, tatizo ni CCM
ii)           Kila kwenye msafara wa mamba na kenge wamo
Uongozi unamwakikishia Mr Christopher Lukosi kwamba mamba wote wa CHADEMA UK kwa kushirikiana na wote wenye kuelewa mageuzi ya kweli, tutaliondoa tatizo ifikapo 2015. Tunamtakia kila la kheli katika maisha na ni imani yetu tutaendelea kuwa ndugu yake baada ya tatizo kutatuliwa !!!!.
“We fail in most of our endeavours because we too often underestimate People’s Power” [M4C UK, 2012]

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU