CHANGIA HARAKATI

Tawi la Chedema UK limekusudia kukusanya £ 20,000/-  kufikia Mwezi Disemba Mwaka 2012, fedha kwa ajili ya kusaidia kampeni ya M4C na kuchangia huduma za afya Tanzania.  Tunakusudia kununua vifaa mbalimbali kwa ajili ya uhamasishaji wa kampeni kama vile Baiskeli, Pikipiki pamoja na magari ya bei nafuu ili kuwafikia watu wengi zaidi  hususani wananchi waliopo vijijini. Pia tumedhamilia kuchangia  huduma za afya nchini kwa kununua vifaa mbalimbali vya huduma ya afya ili kuboresha utoaji wa huduma za afya mahospitalini.

Ili kufikia malengo yetu tunawaomba Wanachama, Watanzania na Wadau mbalimbali wanaopenda mabadiliko na maendeleo ya nchi yetu kuchangia na kushirika katika harakati hizi za mabadiliko ya kweli.

Pia unaweza kushiriki kwa kuandaa fundraising mbali mbali  kama vile Matembezi, mbio, Chakula, Pati, Matamasha ya Muziki na Burudani n.k

Kwa maelezo zaidi na Kuchagia tutumie barua pepe kupitia chademauk@gmail.com

No comments:

Post a Comment

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU