Sunday 30 September 2012

John Heche afichua mbinu chafu zinazoelekezwa kwa Chadema


 
Mpango wa kusitisha M4C, baada ya ccm kugundua kwamba mbinu zote za kusitisha M4C kwa kutumia polisi na dola zimegundulika baada ya kujaribu kutumia vifo vya Morogoro na Iringa kushindikana sasa wameamua kuwatumia CUF, mpango unaonyesha kwamba CUF watakwenda kwenye maeneo ambayo chadema ina nguvu kubwa sana kama Arusha, Mbeya, Mwanza, Manyara, Kiliman jaro,morogoro, Shinyanga,Mara na maeneo mengineyo
 
 

Mbali na hilo watafanya mikutano ambayo itakua na lugha za matusi na kejeli na kuikashfu Chadema na viongozi wake ili wapenzi na wanachama wa chadema wawafanyie fujo hao wanaotukana au watumie watu watakaovalishwa nguo za chadema kuanzisha fujo kwenye mikutano ya CUF ili ionekane kwamba CUF wanafanyiwa fujo baada ya kuoneka hivyo Cuf watawataka wanachama wao pia kuifanyia chadema fujo na hivyo serikali itaingilia kati kufuta operesheni M4C na kile kilichoanzishwa na CUF kwa jina la V4C na malengo ya ccm kutuzuia kwenda vijijini kuwaamshaWatanzania yatatimia kwa kutumia justification kwamba mikutano hiyo inafujo kwahiyo imefutwa au kusitishwa na hapo CUF watakubali kwa haraka maana ni mpango wa pamoja, nachukua fursa hii kuwaomba vijana wa Chadema popote walipo wasifanye fujo au hata kutukana mtu hata wakifanyiwa fujo wasijibu maana tutawapa fursa wabaya wetu kutumaliza, tunaikaribisha sana CUF popote ili wajipime na kuona je ni washindani wetu kweli? sisi hatushindani na CUF wala chama kingine chochote cha upinzani bali adui yetu ni ccm, ninawaomba viongozi wa vyama vya upinzani hasa Cuf kuacha kutumiwa na dola kufifisha harakati za watanzania kuleta mabadiliko ya kweli katika nchi hii kwa kutumia chama chao cha demokrasia na maendeleo chadema.

MUNGU IBARIKI CHADEMA, MUNGU IBARIKI TANZANIA, HAKUNA KULALA MPAKA KILEWEKE

No comments:

Post a Comment

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU