Thursday 6 September 2012
Tuesday 4 September 2012
CHADEMA UK KUUNGURUMA MILTON KEYNES
BAADA YA KUISAMBARATISHAccm READING, WIMBI LA MABADILIKO YA LAZIMA SASA KUUNGURUMA MILTON KEYNES
TAWI LA UK
TUNAWATANGAZIA WATANZANIA WOTE WAISHIO MILTON KEYNES NA MIJI YA JIRANI
KUWA KUTAKUWA NA MKUTANO UTAKAOFANYIKA
TAREHE 15/09/2012 KUANZIA SAA SABA MCHANA MPAKA SAA KUMI NA MBILI JIONI
TUTAWAJULISHA BAADAE KUHUSU UKUMBI
MNAKARIBISHWA MJIUNGE NA HARAKATI ZA KUENEZA DEMOKRASIA YA KWELI NCHINI KWETU
HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE
SISI SOTE NI NDUGU TATIZO NI CCM
Kutakuwa na usafiri kutoka London na Reading
REFRESHMENTS WILL BE AVAILABLE
kwa taarifa zaidi, tafadhali wasiliana na wafuatao:-
Mwenyekiti: Mr CHRIS LUKOSI - 07903828119
&
Mwakilishi wa Reading: Mr GERALD LUSINGU
PEOPLE'S POWER
Sunday 2 September 2012
Matukio mbalimbali katika mkutano wa M4C Reading
Mwenyekiti Mh Likosi Akihutubia Mkutano |
Katibu wa Chadema UK Kamanda Liberatus Musiba akiwa na Mwenyekiti wakifuatilia mkutano |
Mh Lukosi na Mweka Hazina Dr Alex wakimsikiliza kwa makini Kamanda Godbless Lema akihutubia mkutano huo kwa njia ya simu |
Dr Alex Paurine ambaye pia ni Mweka hazina akihutubia mkutano huo, Dr Paurine alitumia Power Point kuonyesha picha na matukio yanayoonyesha hali halisi ya maisha ya Watanzania wengi. |
Ndg Aseri Katanga Mwenyekiti wa bodi ya Computer for Africa akihutubia |
Gerald Lusingu, Mmoja wa wenyeji wa Mkutano wa M4C Reading na aliyechaguliwa kuwa mwakilishi wa M4C Reading akiwasalimia wananchi |
Dr Lusingu akitoa Historia ya Harakati za Mabadiliko na Mageuzi katika nchi yetu, huku akifuatiliwa kwa makini na Katibu wa wanawake Bi Margaret Malekia, Katibu Mh Liberatus na Mwenyekiti Mh Lukosi |
Engineer Prudence Kahatano akichambua matokeo ya azimio la Zanzibar lililovunja azimio la Arusha na madhara ya soko huria kwa Watanzania |
Wadau Mbalimbali katika Mkutano
Wanachama mbali mbali wakikabidhiwa kadi za Chadema na Mwenyekiti wa Chadema UK Mh Chriss Lukosi
Ndg Wambura akivalishwa Gwanda na Kupewa kadi ya Chadema na Mwenyekiti Mh Lukosi |
Saturday 25 August 2012
TAARIFA YA USAFIRI KWENDA M4C READING
TAWI LA CHADEMA UK LINAPENDA KUWATANGAZIWA WANACHAMA WAKE WOTE, WATANZANIA WOTE NA WAPENZI WA CHADEMA WAISHIO LONDON KUWA WAWASILIANE NA CHRIS LUKOSI KWA TARATIBU ZA USAFIRI WA KWENDA READING KUHUDHULIA MKUTANO WA M4C.
MAGARI YATAONDOKA SAA NNE ASUBUHI
Mkutano utafanyika siku ya Tarehe 26/08/2012 kuanzia saa saba mchana mpaka saa kumi na mbili jioni, siku ya Bank Holiday. Risc Reading International Solidarity Centre, 35-39 London Street, Reading, RG1 4PS .
WASOMI WENGI NA WANAHARAKATI MBALI MBALI WATAONGEA SIKU HIYO,
SIKU YA MKUTANO TUTAANZISHA MFUKO WA KUFA NA KUZIKANA KWA AJILI YA WATANZANIA WOTE WAISHIO UK BILA KUBAGUA CHAMA CHAKO CUF,CCM,UDP,TLP WOTE MNAKARIBISHWA
Watanzania wote na wadau mbali mbali mnakaribishwa
SISI SOTE NI NDUGU, TATIZO NI CCM
ni wakati wa kusimama na kusema tumechoka
KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA HAWA WAFUATAO
MWENYEKITI: Chris Lukosi 07903828119
Au tutumie email kupitia chademauk@gmail.com
Peooooople's Power
Friday 24 August 2012
Dk. Slaa: CCM wana sababu za kikoloni
KATIBU Mkuu wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ), Dk. Willibrod Slaa, amesema kuwa Chama Cha
Mapinduzi (CCM), kinachukiwa na wananchi kutokana na kuendelea kujitetea kwa
kutumia sababu zilizotumiwa na wapigania uhuru wa Tanganyika kujikomboa katika
mikono ya wakoloni.
Akizungumza katika mikutano
ya hadhara kwenye vijiji mbalimbali vya kata za Ngerengere na Makambarai, Dk.
Slaa alisema serikali ya CCM imeshindwa kutengeneza fursa ya wananchi kujiletea
maendeleo yao licha ya kuwa katika nchi yenye rasilimali nyingi.
“Mwalimu Nyerere pamoja na
wapigania uhuru wengine wa Tanganyika hawakumkataa mkoloni kwa sababu ya rangi,
dini wala hali zao isipokuwa waliwakataa kwa vile walishindwa kuwaondolea watu
umaskini, ujinga na maradhi ambayo yanaendelea kutuandama kila wakati,”
alisema.
Alisema kuwa hayati Mwalimu
Nyerere alifikia malengo kwa kuonesha njia ya kupita, hivyo waliomfuatia
walikuwa na wajibu wa kuhakikisha njia hiyo inapitika lakini serikali ya CCM
imeamua kuziba njia hiyo.
Huku akisoma takwimu za
maendeleo katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, linaloongozwa na Dk. Lucy
Nkya (CCM), Dk. Slaa alisema kuwa hakuna sababu ya kuendelea kukivumilia chama
hicho kwa sababu ya kufanana kwa rangi na badala yake wananchi wanapaswa
kuchukua hatua ya kukipumzisha.
“Kila mmoja hapa amesikia
takwimu nilizosoma, tena zinatokana na vitabu vya serikali yenu hii mliyoichagua
na kuiweka madarakani, mlichagua rais wa CCM, mbunge wa CCM, Diwani wa CCM,
mwenyekiti wa kijiji na serikali ya kijiji ya CCM, sasa nawasomea hapa ufisadi
unaofaywa mnaanza kusikitika,” alisema.
Alisema ni aibu miaka 50
baada ya Uhuru kusikia Watanzania wakizungumzia upungufu wa madawati wakati nchi
nyingine zikiwa zinashindana kwenda kuangalia uwezekano wa kufanya utafiti
utakaozisaidia nchi zao.
Thursday 23 August 2012
Mwalimu mmoja wanafunzi 652
Akiwa katika Oparation Sangara inayoendelea hivi sasa nchini, Mwenyekiti wa Baraza la vijana la Chadema, Bwana Deogratias Munishi amegundua shule ambayo inawanafunzi 652 na Mwalimu mmoja tu. Shule hiyo ipo katika Kijiji cha Kadodo Kata ya Luale, Mvomelo Mkoani Morogoro. Hii ndo hali halisi ya elimu Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru, chini ya utawala wa CCM.
Mwenye shati la rangi ya udongo na suruali nyeusi ndiye Mwalimu Mkuu na Mwalimu pekee wa Shule ya Msingi Kododo iliyopo kata ya Luale, Mvomelo Mkoani Morogoro. Shule hiyo inawanafuzi 652. |
Aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM kata ya Muhonda akieleza jinsi alivyokunwa na sera za CHADEMA zilizoelezwa na katibu Mkuu wa BAVICHA katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kichangani. |
Wednesday 22 August 2012
Dr. Slaa na Rasilimali za Taifa
Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbrod Slaa amelitaka Jeshi la Polisi kutumia fedha na uwezo wake kulinda Rasilimali za Taifa sio kupambana na CHADEMA
Tuesday 21 August 2012
MAHAKAMA YATENGUA UBUNGE JIMBO LA IGUNGA
Tuesday 14 August 2012
CHADEMA KUWASHA MOTO KATIKA MJI WA READING SIKU YA TAREHE 26/08/2012
UK
Ili kufikia malengo
yetu ya kuzunguka kwenye Miji mbalimbali ya UK kuhamasisha Watanzania waishio
uk kujiunga na Chadema, kueneza kampeni ya m4c na kufungua matawi mengine, Tawi la
Chadema London linapenda kuwatangazia Watanzania wote waishio katika Mji wa
Reading na maeneo ya jirani kuwa kutakuwa na mkutano mkubwa wa M4C UK utakao fanyika Tarehe
26/08/2012 siku ya Bank holiday.
Dhumuni la mkutano huo ni kuwahamasisha Watanzania
waishio UK kujiunga na chama, kushiriki katika harakati za mabadiliko, kusajili
wanachama wapya, kuchagua wawakilishi wa
muda kutoka mji wa Reading pamoja na kuanzisha mfuko wa kufa na kuzikana kwa manufaa
ya watanzania wote.
Tumekusudia
kuanzisha Mfuko wa kufa na kuzikana kwa sababu mpaka hivi sasa Mtanzania
akifariki akiwa UK hakuna taasisi wala
ofisi yoyote inayotoa msaada. Jukumu ambalo kwa muda mrefu Serikali yetu
kupitia ubalozi umelipuuzia na kushindwa kulisimamia na kulishughulikia.
Mfuko huu utasaidia katika kumsafirisha Marahemu na Mfiwa pamoja na kusaidia kushughulikia matatizo na usumbufu utakaojitokeza baada ya mtu kufariki dunia na kusaidia matatizo mbalimbali yakiwemo majanga ya dharura.
Mfuko huu utasaidia katika kumsafirisha Marahemu na Mfiwa pamoja na kusaidia kushughulikia matatizo na usumbufu utakaojitokeza baada ya mtu kufariki dunia na kusaidia matatizo mbalimbali yakiwemo majanga ya dharura.
Pia katika mkutano huo wanachama mbalimbali wa CCM walio na uchungu na nchi yetu na wanaopenda maendeleo na mabadiliko
ya kweli watapewa nafasi ya kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo kama
sehemu moja wapo ya kampeni yetu ya
Kuvua Gamba na Kuvaa Gwanda ukiwa Ughaibuni.
Mkutano utafanyika
siku ya Tarehe 26/08/2012, Kuanzia saa saba mchana mpaka saa kumi na mbii jioni.
Risc Reading International
Solidarity Centre,
35-39 London Street,
Reading, RG1 4PS
Huu ndio wakati wa mabadiliko, kusimama na kusema tumechoka!
KWA
MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA;
MWENYEKITI: Chris Lukosi 07903828119,
MWENYEKITI: Chris Lukosi 07903828119,
Monday 13 August 2012
MATUKIO MBALI MBALI KATIKA SIKU YA UFUNGUZI WA TAWI LA CHADEMA LONDON
VUA GAMBA VAA GWANDA UGAIBUNI
Mhe. Lema na Mwenyekiti wa Muda wa Chadema Lodon Chriss Lukosi wakionyesha baadhi ya kadi na Tshirt zilizorudisha na wanachama wa CCM |
Mmoja aliyekuwa Mwanachama na Mkereketwa wa CCM toka Mwaka 1984 Ndg. Christopher Chegula akirudisha Tshirt na Kadi ya CCM kwa Mhe. Lema |
Mhe. Lema akimkabidhi kadi ya Uanachama wa CHADEMA Christopher Chegula |
Bi. Jessca Maduhu akipokea kadi ya uanachama wa chadema kwa furaha kutoka kwa Lema |
Mwanachama Mpya akikabidhiwa kadi yake |
Jessica akipokea kadi yake ya CHADEMA |
Mmoja ya wanachama waliokabidhiwa kadi na Mh Lema |
Esther baby Cuthbert akionyesha kadi yake mpya ya Chadema |
VIONGOZI WA MPITO WALIOCHAGULIWA KULIONGOZA TAWI LA CHADEMA LONDON
Mkutano wa ufunguzi wa Tawi la Chadema
London ulikwenda sambamba na uchaguzi wa viongozi wa mpito wa Tawi watakao ratibu na kusimamia shughuli mbalimbali za chama kwa muda, uchaguzi uliongozwa na kusimamiwa na Mh Godbess Lema ambaye ni mjumbe wa Baraza Kuu la Chadema Taifa.
Viongozi waliochanguliwa kuratibu na kuongoza shughuli za chama kwa muda ni wafuatao;
Viongozi waliochanguliwa kuratibu na kuongoza shughuli za chama kwa muda ni wafuatao;
Chris Lukosi - Mwenyekiti |
Subscribe to:
Posts (Atom)