Thursday 4 October 2012

Zitto apeleka hoja bungeni kutaka uchunguzi walioficha mabilioni nje

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameiandikia barua Ofisi ya Bunge kuitaarifu nia yake ya kuwasilisha hoja binafsi katika Mkutano wa 11 wa Bunge kuliomba liazimie Serikali iwasiliane na taasisi za kimataifa, hasa benki kusaidia kurejeshwa nchini fedha zote haramu ambazo zimefichwa na Watanzania katika benki za nchini Switzerland na kwingineko duniani.
Taarifa zilizopatikana jana kutoka Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni zimeeleza kuwa Zitto anaomba Serikali ifanye hivyo kwa Benki ya Dunia kupitia taasisi yake ya Stolen Asset Recovery Initiative, kutekeleza jukumu hilo.
Taarifa hizo zimeeleza kuwa katika barua hiyo Zitto anatumia kifungu cha kanuni za bunge namba 55 (1) na (2), na hoja yake itaainisha fedha ambazo Benki ya Taifa ya Switzerland ilitangaza kwamba Watanzania wamezihifadhi, ambazo ni Sh297 bilioni.
Barua hiyo imeainisha kuwa fedha hizo ni sawa na Dola za Marekani 186 milioni na Zitto amebainisha kuwa hoja yake hiyo itaainisha namna na njia ambazo zilitumika kutorosha fedha hizo kwenda katika benki hiyo na nyingine za nje.
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah alikataa kuthibitisha kupokea barua hiyo badala yake alieleza kuwa hilo ni suala la kiofisi.
"Ni suala la ndani la ofisi, siwezi kueleza kama ni kweli nimepokea au la, isipokuwa suala hilo linafahamika na ofisi ya Bunge ililipokea alipoliwasilisha bungeni hivyo linafanyiwa kazi," alisema Kashillilah.
Mapema mwaka huu, baadhi ya vyombo vya habari likiwamo gazeti hili, vilifichua kuwapo kwa fedha zilizofichwa nchini Uswisi na baadaye ilibainika kwamba fedha hizo ni mali ya Watanzania 27 wakiwamo wanasiasa na wafanyabiashara.
Gazeti hili pia lilibaini kwamba mmoja wa walioficha fedha hizo anamiliki Dola za Marekani milioni 56 (sawa na Sh89.6 bilioni).
Katika uchunguzi wake, Mwananchi limebaini pia kuwa kiasi cha fedha kilichothibitishwa kumilikiwa na Watanzania hao ni jumla ya Dola za Marekani 186 milioni (takriban Sh300 bilioni) kwa viwango vya sasa vya kubadilishia fedha ambavyo ni Sh1600 kwa Dola ya Marekani.
Taarifa hizo zinaeleza kuwa mbali na kigogo anayemiliki Sh90 bilioni, wapo wengine wanne, ambapo anayefuatia anamiliki Dola 30 milioni (Sh48 bilioni), mwingine Dola 20 milioni (Sh32 bilioni) na wengine wawili kila mmoja anamiliki Dola 10 milioni (Sh16 bilioni).
Kwa kuangalia fedha hizo ni dhahiri kwamba vigogo watano tu kati ya kundi la Watanzania 27, wanamiliki Dola 126 milioni (Sh201.6 bilioni) sawa na asilimia 67.74 ya fedha hizo, wakati wengine 22 waliobaki wanamiliki Dola 60 milioni (Sh96 bilioni) sawa na asilimia 32.25.
Habari hizo zilikuwa zikinukuu taarifa ya Benki Kuu ya Uswisi iliyoitoa na kuonyesha kuwapo kwa kiasi cha Sh315.5 bilioni zilizotoroshwa Tanzania na kufichwa nchini humo na vigogo ambao ni wanasiasa pamoja na wafanyabiashara.
Mwananchi

Wednesday 3 October 2012

Vigogo CCM ‘wahamia’ Marekani

• Ni JK, Mkapa, Kinana, Membe na Nape
 
VIGOGO watano wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wako nchini Marekani, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Uwepo wa vigogo hao Marekani kwa wakati mmoja, umeibua gumzo nchini hususan kwa mitandao ya makada wa chama hicho wanaotajwa kutaka kuwania urais mwaka 2015.
Vigogo hao ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, na mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC), Abdulhaman Kinana, ambaye amepata kuwa kampeni meneja wa marais hao wawili.
Mwingine ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, ambaye amekuwa akitajwa kuwa mmoja wa makada watakaowania urais mwaka 2015.
Wakati vigogo hao wako nchini Marekani, kigogo mwingine wa CCM, Nape Nnauye, ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, anatarajia kwenda nchini Marekani kesho.
Ingawa vigogo hao wako Marekani kwa shughuli na sababu tofauti, mahasimu wa Waziri Membe kisiasa wamehusisha ziara hiyo ya wazito hao na harakati za urais 2015.
Rais Kikwete yuko nchini Marekani kwa ziara ya kikazi. Rais na ujumbe wake uliondoka nchini juzi na atakuwa hapo kwa siku mbili kabla ya kuelekea nchini Canada kwa ziara nyingine rasmi ya kiserikali.
Habari zinasema kuwa Mkapa na Kinana waliondoka nchini wakati vikao vya mchujo vya CCM vikiendelea mjini Dodoma na wako nchini humo kwa ajili ya shughuli za taasisi ya Mkapa Foundation na Nape anatarajia kwenda kwa shughuli zake binafsi.
Hadi sasa hakuna kada yeyote wa CCM aliyetangaza kuwania urais, lakini mbali ya Membe, duru za kisiasa zinawataja makada wengine wanaotaka urais kuwa ni pamoja na mawaziri wakuu wastaafu, Frederick Sumaye na Edward Lowassa.
Hata hivyo, kasi ya Sumaye kuwania nafasi hiyo imepunguzwa na matokeo ya uchaguzi wa NEC, wilayani Hanang’ ambapo aliangushwa na Dk. Mary Nagu.
Wengine ni Samuel Sitta, Dk. Abdallah Kigoda, Dk. Emmanuel Nchimbi, Dk. Asha Rose Migiro na wengine.
KWA HABARI KAMILI TEMBELEA:
 

Kingunge nusura amng’oe Kikwete

MWENYEKITI wa Chama cha Mapunduzi, Rais Jakaya Kikwete, na sekretarieti yake wameponea tundu la sindano kung’oka baada ya mkongwe wa siasa nchini, Kingunge Ngombale Mwiru, kutangaza mgogoro wa katiba ya chama hicho ambao ungehatarisha nafasi yake.
Kingunge ambaye ameshika nafasi mbalimbali za uongozi nje na ndani ya chama, aliwasilisha hoja hiyo ya mgogoro wa katiba wiki iliyopita wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), iliyokuwa na ajenda ya kufanya uteuzi wa majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM.

CCM KWA WAKA MOTO

Sumaye amtangazia vita Lowassa
• Mwenyewe asema wananchi wa Monduli ndiyo msuli wake

CCM KWA WAKA MOTO

 
Lowassa awatimulia vumbi Sitta, Membe
 
APANGA MAJESHI YA URAIS 2015, ASEMA MONDULI NDIYO MSULI WAKE WA KISIASA

Rufani Ya Lema Yatikisa Arusha


Video Rufaa ya Godbless Lema
 
Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema akiwahutubia wafuasi wake baada ya Jaji MKuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman kuahirisha kesi ya rufaa ya aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.Picha Zote na Jackson Odoyo Mussa Juma, Arusha MAWAKILI wanaomtetea aliyekuwa Mbunge wa Arusha, Godbless Lema wamedai mbele ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kuwa mteja wao yuko huru kwa kuwa mahakama haikutengua ubunge wake.Katika kesi hiyo, Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande anawaongoza wenzake wa Mahakama ya Rufani, Salum Massati na Natalia Kimaro kusikiliza maombi ya rufani hiyo, inayopinga Lema kuvuliwa ubunge.

Mawakili hao wa Lema jana walitoa hoja ya kupinga hukumu hiyo kufuatia mabishano baina yao na upande wa utetezi kwa maelezo kuwa taratibu za ufunguaji wa rufaa hiyo zimekosewa. Awali wakili Alute Mughwai aliiomba mahakama hiyo kutupilia mbali rufani hiyo kwa kile alichoeleza kuwa ina upungufu mwingi wa kisheria na kikanuni. Wakili huyo alitaja baadhi ya kasoro za rufani hiyo kuwa ni hati ya kukaza hukumu (tuzo) ambayo imewasilishwa mahakamani hapo kutokuwa na mhuri wa Jaji Gabriel Rwakibarila aliyetoa hukumu ya kesi hiyo.
Alidai kuwa katika rufani hiyo pia kuna upungufu kuhusu tarehe za kuwasilishwa kwa rufani, pia baadhi ya vifungu vimekosewa.Wakili Mughwai alitoa kumbukumbu ya kesi kadhaa ambazo mahakama ya rufani ilizitupa baada ya kukosa hadhi ya kisheria kusikilizwa.

“Mawakili wa Lema walipaswa kabla ya kuwasilisha mahakamani rufani yao, kujiridhisha kama kuna upungufu katika nyaraka ambazo wanawasilisha mahakamani.”Alisema kubwa katika makosa ambayo amebaini katika rufani hiyo ni kuwasilishwa bila kuwekwa mhuri hati ya kukaza hukumu (tuzo) iliyotolewa na Jaji aliyetoa hukumu katika kesi ya awali.“Hapa nani ambaye anajua sahihi ya Jaji? Alihoji. Hawa mawakili walipaswa kushinikiza kuwekwa mhuri wa mahakama katika hukumu hiyo ili kuthibitisha uhalali wake,” alisema Alute. Hata hiyo, wakili huyo alisema badala yake, mawakili hao waliwasilisha mahakamani rufani hiyo ndani ya siku 29 tu baada ya hukumu, badala ya siku 60 ambazo walipewa.

Kwa kuwasilisha mahakama ya rufani, hukumu ambayo bado haina mhuri wa Jaji ni ukiukwaji wa kanuni na taratibu za mahakama.”Mughwai alidai kuwa katika mazingira ya sasa hakuna cha kurekebishwa katika rufani hiyo, badala yake itupwe na kuwataka wakata rufani kulipa gharama zote za kesi. Hata hivyo, hoja hizo zilipingwa na mawakili wa Lema ambao ni Tundu Lissu na Method Kimomogoro, ambao walidai kuwa hawakuwa na mamlaka ya kumlazimisha Jaji Rwakibarila kuweka mhuri.

Lissu alidai "Kama inaonekana sasa kuwa ni batili, basi hata uamuzi wa kumvua ubunge Lema ni batili," alisema. Wakili Kimomogoro Kwa upande wake, Wakili Kimomogoro alisema kisheria kasoro hizo ya mhuri wa mahakama na tarehe, haziwezi kusababisha rufani hiyo kutupwa kwani haziathiri madai ya msingi katika rufani.

Alidai kesi hiyo ya Lema ilikuwa ya kipekee kwani mara tu baada ya hukumu kutolewa faili lilipelekwa jijini Dar es Salaam na maombi ya nyaraka kadhaa za kesi hiyo yalitumwa kutoka Dar es Salaam.“Katika mazingira kama haya hatuwezi kuepuka makosa ya kibinadamu ambayo yanatambulika kisheria,” alidai Kimomogoro. Aliongeza kuwa katika hoja hiyo, waliandika kifugu namba 114 badala ya 113 kimakosa ya kiuchapaji, lakini hakipotoshi kitu chochote kwani kifungu hicho hakipo. Wakili Kimomogoro alisema wakili mwenzake, Mughwai ameshindwa kuzungumzia uamuzi ya kesi ambazo, hazikufutwa kutokana na kuwa na upungufu mdogo wa aina hiyo ambao kimsingi hauathiri rufani. Hata hivyo, alisema kama wakili huyo alibaini makosa hayo, katika uwasilishaji wa hoja zake, alipaswa pia kurekebisha kwa mujibu wa sheria ya mwaka 2009 ya mahakama. Kimomogoro pia aliwasilisha mahakamani hoja kadhaa za kisheria na uamuzi ya Mahakama ya Rufani za ndani na nje ya nchi, ambazo hazikutupilia mbali rufani ambazo zilikuwa na upungufu mdogo, kwani lengo la mahakama hizo ni kutafuta haki.
“Siyo kila kasoro au usumbufu kwenye hukumu unaweza kusababisha kutupwa rufani kwani kasoro zote zilizotajwa ni za makosa na uchapaji na nyingine ni za kiutaratibu tu,” alisema. Alifafanua kuwa makosa ambayo yanaweza kusababisha rufani kutupwa ni kama aina namba ya kesi, majina na wadhifa wa wadau katika shauri husika, mambo yanayolalamikiwa na mahakama imeamua nini.

Wakili huyo alifafanua kuwa jambo la kukosekana mhuri wa mahakama wa Jaji siyo kubwa na kusababisha kutupwa rufani kwani hakuna ambaye anapinga hukumu iliyowasilishwa mahakamani. Kwa upande wake, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Vitalis Timoth alisema anaunga mkono hoja za mawakili wa Lema, kuwa pingamizi ya wakili Mughwai haina msingi wa kisheria.

Alisema hati ya kukaza hukumu (Tuzo) inatolewa chini ya sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai na siyo chini ya sheria ya masijala za mahakama. Alisema siyo kazi ya jaji aliyetoa hukumu, kuweka mhuri hukumu yake bali hiyo ni kazi ya msajili wa mahakama na masijala za mahakama.

Kama hati ya kukaza hukumu ina matatizo anayepaswa kulaumiwa siyo mawakili bali ni mahakama ambayo ndiyo ilikuwa na mamlaka ya kuweka mhuri,” alisema. Alidai kuwa pingamizi ya awali ya rufani inapaswa kuwa na sifa mbili, kwanza iwe na suala la kisheria na pili iendane na kesi ya msingi.“Katika hoja za wakili Mughwai ni wazi inathibitika pingamizi hili halina matakwa ya kisheria kwani hata kama ikipitwa siyo kuwa itazuia kurejeshwa tena na kusikilizwa kwa rufani ya msingi.”Alidai ni busara kuacha kuwa na pingamizi ambazo zinaongeza gharama za kesi na muda wa kusikiliza.

Ushauri wangu kila shauri liamuliwe kwa mazingira yake na uamuzi wa sasa uzingatie mahakama katika kutenda haki,” aliongeza. Alidai kwamba kutupwa kwa hoja ya kutaka waomba rufani wachapwe mijeledi kwani kazi ya mahakama siyo kuchapa watu bali ni kutoa haki.“Tunashauri kusikilizwa rufani kwa kuzingatia sheria na ushahidi,” alisema. Jopo la Majaji Baada ya kutolewa kwa hoja za pande zote za mawakili, Jaji Chande na Jaji Massati waliwauliza maswali kadhaa mawakili hao na kujieleza na baadaye Jaji Chande alitangaza kuahirishwa kwa kesi hiyo hadi hapo itakapotangazwa. Jaji Chande alisema vikao vya Mahakama ya Rufani Kanda ya Arusha vimemalizika jana, hivyo uamuzi wa kutupwa kwa pingamizi la rufani hiyo au la utatolewa siku itakayopangwa na mahakama.

Baada ya uamuzi huo umati wa wafuasi wa Chadema, uliokuwa ndani na nje ya mahakama ulianza kuimba nyimbo mbalimbali kama vile Lema Jembe na bila Lema patachimbika. Katika hatua ya kuepuka vurugu, Lema alizungumza na wafuasi hao nje ya mahakama na kuwataka kuondoka kwa amani kwenda katika ofisi ya Chadema iliyopo Ngarenaro kwa amani bila vurugu.

Warufaniwa katika kesi hiyo ni makada wa CCM, Happy Kivuyo, Mussa Mkanga na Agnes Mollel ambao walishinda kesi ambayo hukumu yake ilimvua ubunge Lema Aprili 4, mwaka huu.


 Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari

Tuesday 2 October 2012

VIONGOZI WA BAVICHA TAIFA WAALIKWA KUHUDHURIA MKUTANO MKUU WA BARAZA LA VIJANA LA CHAMA TAWALA NCHINI UJERUMANI


Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa John Heche na Katibu Mkuu wake Deogratius Munishi wamealikwa na Baraza la vijana la chama tawala nchini Ujerumani kuhudhuria mkutano wake mkuu.
Vijana hao wa BAVICHA wamealikwa kama wawakilishi kutoka Tanzania na Africa kwa ujumla.Pia wamepewa heshima kubwa ya kuhutubia mkutano huo mkuu.
Mkutano mkuu huo utahudhuriwa na Chancellor wa Ujerumani Bi. Angel Markel.

RUFAA YA MH. GODBLESS LEMA YAAHIRISHWA Yapigwa ‘Kalenda’

 
Kwa mwendelezo wa jinsi kesi iliyokuwa mahakamani na maoni ya watanzania mbalimbali tembelea:  http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/331912-live-updates-mwendelezo-wa-kusikilizwa-rufaa-ya-lema-oktoba-02-2012-a.html

M4C yazoa makada 201 wa CCM kwa Dk. Magufuli

 
Mikutano ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) inayofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilayani hapa, Mkoa wa Geita, imezoa makada 201wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwamo Mwenyekiti wa
Kitongoji cha Buhungu, Kata ya Kigongo.

Makada waliotimkia Chadema kutoka Jimbo la Chato linalowakilishwa na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kwa nyakati tofauti, wanatoka katika Kijiji cha Muganza, Kasenga, Busaka na Igando, Kata ya Bwera, ambako chama hicho kimefanya mikutano ya hadhara.

WanaCCM hao walidai wamekihama chama hicho kwa sababu wamechoshwa na mwenendo wa siasa zake, walizodai zimechangia maisha ya wananchi kuwa magumu.
CHANZO: NIPASHE

Mbunge awachochea wananchi Karatu

 
MBUNGE wa Karatu, Mchungaji Israeli Natse (CHADEMA), amewahamasisha wananchi wake wa Kata ya Baaray, Tarafa ya Eyasi kuwacharaza viboko watendaji wa vijiji na kata kutokana na tuhuma za kuchukua rushwa na kuruhusu wafanyabiashara wa vitunguu kukata miti na kulima katika chanzo cha maji cha Qangded.
Mchungaji Natse alitoa kauli hiyo juzi wakati akihutubia wananchi katika Kijiji cha Jobaj ambacho ni miongoni mwa vijiji saba vinavyotegemea chanzo hicho cha maji.
Alisema uamuzi wa kuwacharaza viboko watendaji hao, unatokana na ulegelege unaoonyeshwa na Serikali ya Rais Jakaya Kikwete katika kusimamia sheria na kanuni za utumishi.
Mchungaji Natse yupo jimboni akiambatana na wabunge wengine na viongozi kadhaa wa CHADEMA kutembelea vijiji mbalimbali kuangalia sakata la uharibifu wa mazingira lililofanywa na wafanyabiashara katika bonde la Mto Eyasi.
Wabunge wengine alioambatana nao ni Kabwe Zitto (Kigoma Kaskazini), Rose Kamili (Viti Maalum), Tundu Lissu (Singida Mashariki), Pauline Gekul (Viti Maalum) na Joshua Nasari (Arumeru).
Akiwahutubia wananchi katika vijiji saba vinavyozunguka bonde hilo la Eyasi, Natse alisema uharibifu huo unachangiwa kwa kiasi kikubwa na udhaifu wa Serikali ya Rais Kikwete.
Natse alieleza kuwa uharibifu uliofanywa na wafanyabiashara watano katika vyanzo hivyo vya maji katika bonde la Ziwa Eyasi, ulianza kushughulikiwa vizuri na Mkuu wa Wilaya hiyo, Daudi Ntibenda kwa kuwakamata waharibifu hao, lakini maagizo ya kichama yaliyotolewa na kuongezwa shinikizo la Mkuu wa Mkoa wa Arusha, yalifanya watuhumiwa hao kuachiwa bila masharti.
Alisema hali hiyo inatokana na ulegelege wa Serikali ya Rais Kikwete ambapo watumishi wake wa ngazi za kati na chini wanajiamulia mambo bila kujali madhara ya uamuzi huo wanaoufanya kwa wananchi na hata kwa chama chao cha siasa wanachokitumikia.
“Naomba Kikwete anisikie na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo. Ulegelege wa serikali hii ndio unaotaka kuhatarisha maisha ya wakazi wanaozunguka bonde hili kwa kuwalinda wafanyabiashara wa vitunguu waliofyeka miti katika vyanzo vya maji na wao kuweka mashine 32 za kuvutia maji kwenda kwenye mashamba yao kwa kuwa wanaifadhili CCM,” alisema Natse.
Alifafanua kuwa wanatoa muda wafanyabiashara hao waondoke wenyewe kabla harakati hazijaanza kwa kutumia wananchi kuwatoa hapo kwa kuwa hakutakua na woga wa mabomu ya machozi wala virungu vya polisi wakati wa kuwaondoa.
Watuhumiwa wanaotajwa kuhusika na kuharibu chanzo hicho kikuu cha maji ni katika Kata ya Mang’ola ambao walikamatwa na mkuu wa wilaya na kuwekwa rumande kabla ya kuagizwa kuwaachia huru ni Waziri Saidi, Christopher Msemo, Loema Gilong, Girigisi Gidobad, Mamoya Muhindi na Sudi Omary.
Naye Kamili akihutubia wakazi wa Kijiji cha Jobag, aliwahamasisha kutozubaa kwa kuwa wao ndio wataathirika wa uharibifu huo, hivyo akawataka akina mama na vijana kufunga vibwebwe na kuhamia katika vyanzo hivyo kuondoa mashine hizo na kulilinda eneo hilo kwa muda wote.
Tanzania Daima

Zitto, Lissu wang’aka Karatu

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto na mwenzake wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), wamewaonya viongozi na madiwani wa chama hicho wilayani Karatu kuwa hawatavumiliwa endapo watashindwa kutatua tatizo la maji wilayani humo.
Vigogo hao walitoa msimamo huo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wakiwahutubia wakazi wa mji wa Karatu wakiwa wameongozana na Mbunge wa jimbo hilo, Mchungaji Israel Natse, katika mkutano wa kuhamasisha maendeleo pamoja na ushiriki wa wananchi katika utoaji wa maoni ya Katiba mpya.
Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara, alisema akiwa kama kiongozi wa chama pamoja na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Lissu, wametoa maagizo kwa viongozi wao wa wilaya chini ya Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Lazaro Maasai, kwenda kuzungumza na wananchi kwenye vijiji ambavyo mradi wa maji wa Kaviwasu unapita.
Alifafanua kuwa lengo la kwenda kuzungumza na wananchi hao ni kujua matatizo yaliyopo ambayo yanasababisha mradi huo kutotoa huduma kwa kiwango kilichokusudiwa na kuyapatia ufumbuzi mara moja ili watu waendelee kupata maji safi na ya kutosha.
“Naomba niwambie wazi kama hawatatekeleza maagizo haya tutawafukuza wote kwa kuwa hatutakubali kuona mradi huo wa maji ulioasisiwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, wakati akiwa mbunge wa jimbo hili unaharibiwa na watu wachache wenye tamaa ya fedha,’’ alisema.
Aliongeza kuwa wametembelea maeneo hayo na kukutana na malalamiko mengi juu ya viongozi kushindwa kusimamia vema majukumu yao na kuwataka wananchi wawaambie viongozi hao kuwa katika miradi ya maendeleo hakuna siasa na ikibidi wawawajibishe kama watashindwa kutekeleza majukumu yao.
Akizungumzia kuhusu utoroshwaji wa fedha nje ya nchi unaofanywa na baadhi ya watendaji wa serikali, Zitto alisema tayari wana orodha ya Watanzania 27 ambao wanamiliki mamilioni ya dola nje ya nchi ambayo waliyapata kwa njia zinazotia shaka.
Zitto alitaja kuwa miongoni watuhumiwa hao yumo ofisa mmoja wa jeshi mstaafu ambaye hata hivyo hakumtaja jina, akisema anamiliki akaunti nje ya nchi ikiwa na kiasi cha dola milioni 56.
Aliitaka serikali iwataje wote wanaomiliki fedha nje na kuchukua hatua haraka, vinginevyo wao watawaweka hadharani kwa umma ili nguvu ya wananchi ichukue mkondo.
Naye Lissu akizungumza katika mkutano huo, aliwaonya wananchi wa Karatu wasikubali kuanza kurubuniwa kwa kuchukua visenti vidogo vidogo na kuharibu historia yao nzuri ya mfano kwa nchi hii.
Alisema vitendo vya kuendekeza njaa katika masuala ya utendaji si desturi na mfumo wa chama hicho, hivyo kuwatahadharisha wananchi kuwa kama kunatokea kiongozi ama mwanachama ana matatizo hayo basi hakuna kufichaficha waelezane hadharani.
Kuhusu utoaji maoni kwenye tume ya Katiba, Lissu aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kama wanavyojitokeza kwenye mikutano ya chama hicho ili kutoa maoni yao.
“Naomba niwaambie wananchi nyie mna historia kubwa toka nchi inapata uhuru mliishawahi kuchagua kiongozi bila kupitia chama chochote, Chifu Sarwatt na mkambwaga mgombea wa TANU lakini leo miaka 50 ya uhuru tunaambiwa bado hatujakomaa kuwa na wagombea binafsi, kwa kutumia uandikwaji wa Katiba mpya jitokezeni mtoe maoni yenu,” alisema Lisu.
Alifafanua kuwa wasipojitokeza kutoa maoni kwa tume hiyo watakuwa wamechangia kuruhusu watu wachache kuwaandikia Katiba ama vipengele vingi vya Katiba ya zamani inayolalamikiwa vitabaki vilevile.
Tanzania Daima

KATUNI


WATOTO WA WASIRA WATOA UFAFANUZI JUU YA WAO KUJIUNGA NA CHADEMA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI UFAFANUZI KUHUSU SISI KUJIUNGA NA CHADEMA NA MALUMBANO KUHUSU MAJINA YETU


Tarehe 30/09/2012 mimi Esther Wasira na dada yangu Lilian Wasira tulijiunga na CHADEMA na kukabidhiwa kadi na Katibu Mkuu wa CHADEMA Mh. Dr Willibrod Slaa. Tulielezea kwa kirefu sababu za sisi kujiunga CHADEMA na tukasisitiza kuwa tumeridhika kuwa CHADEMA ni chama chenye dhamira safi ya kuiongoza Tanzania na kwamba ni chama kinacholeta matumaini mapya ya kuijenga Tanzania mpya yenye neema. Waandishi wa habari walijaribu sana kutudodosa kujua tuna uhusiano gani na Waziri Steven Wasira. Tulielezea wazi kuwa mahusiano yetu ya kifamilia hayahusiki na sababu na dhamira yetu ya kujiunga CHADEMA. Hata hivyo tulielezea kuwa Waziri Steven Wasira ni baba yetu mdogo ambaye alinyang'anyana ziwa na baba yetu mzazi, wakili George Wasira. Tulidhani hiyo ilitosha na lisingekuwa swala tena la kujadili na badala yake hoja ya kujadiliwa ingeweza kuwa sababu tulizozieleza za kujiunga CHADEMA. Tunasikitishwa sana na malumbano yaliyofuata baada ya hapo kuhusu kama sisi ni watoto wa Wasira au la. Kama tulivyoeleza, tumejiunga CHADEMA kwa sababu tulizozieleza hapo awali na wala si kwa sababu nyingine yeyote. Hatujajiunga CHADEMA kumdhalilisha mtu, kumfedhehesha mtu au kukipatia umaarufu CHADEMA kwa vile tu tunatumia jina la Wasira. CHADEMA ni chama cha siasa tena chenye wanachama na wafuasi wengi Tanzania hivyo si kashfa bali ni fahari kubwa mtu kujiunga CHADEMA na tena ni ushahidi wa mtu kujitambua. Pia CHADEMA ni Chama maarufu sana Tanzania kwa sasa hata pengine ni maarufu kuliko CCM hivyo hakihitaji kujipatia umaarufu kwa mgongo wetu. Sisi tunawaheshimu sana wazee wetu na tutaendelea kuwaheshimu ila linapokuja swala la chama cha kujiunga linabaki kuwa hiari yetu kwa kuzingatia sera za chama na uwezo wa chama husika katika kujenga Tanzania tunayoitaka na hilo ndilo lililotupeleka CHADEMA. Na hii ni haki yetu ya msingi kabisa inayolindwa na Katiba ya nchi hii chini ya ibara ya 20(1). Ikumbukwe kuwa mmoja wa Waanzilishi wa CHADEMA ni Mzee Wasira. Dhamira ya kuanzisha CHADEMA ilikuwa ni kushika dola na hili ndilo CHADEMA imekuwa siku zote inajaribu kuwashawishi Watanzania kuwa sasa wamekomaa na wanastahili kuchukua dola. Kwa vile kuchukua dola ilikuwa ndio ndoto ya baba yetu mzazi Mwanzilishi wa CHADEMA, sisi kama watoto tumejiunga na M4C ya CHADEMA ili tuweze kutimiza ndoto ya baba yetu kuwa CHADEMA siku moja ichukue jukumu la kuiongoza Tanzania.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:   
Lilian Wasira 0719 604156   
Esther Wasira 0655 048797

Sunday 30 September 2012

Mbowe afichua siri mgogoro wa RC, madiwani Moshi

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema mvutano uliopo kati ya madiwani wa Manispaa ya Moshi na Mkuu wa Mkoa (RC) wa Kilimanjaro ni mpango wa serikali kutotaka kuziachia halmashauri zinazoongozwa na chama hicho kufanya kazi zake mipango iliuyojiwekea.
Mbowe alisema kuruhusu wakuu wa serikali kupindisha maamuzi ambayo yamefanywa na vyombo hivyo vilivyopo kisheria, ni kujenga utawala wa kiimla katika taifa kwa kujiongoza kwa matamko au mapenzi ya viongozi badala ya kanuni za halmashauri.

Alisema kisheria Baraza la Madiwani linajiendesha kwa kanuni na sheria, kwa mamlaka walizopewa madiwani na wananchi, hivyo wakuu wa wilaya na mikoa wanapaswa kuviheshimu vikao hivyo na siyo kuruhusu kutumika na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuvuruga upinzani hata kwa kuvunja kanuni.


Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hai na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, alisema mvutano uliopo sasa katika Baraza la Madiwani linaloongozwa na CHADEMA na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, ni ushuhuda mwingine wa matumizi yaliyovuka mipaka ya kimadaraka ambayo yamekuwa yakifanywa na wakuu wa wilaya na mikoa kuvuruga halmashauri zinazoongozwa na CHADEMA.


“Ndiyo maana sisi kama CHADEMA tunasema kuwa suluhu ya matatizo haya yote ni katiba mpya, kwani cheo cha mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya ni vyeo vya kufutilia mbali, kwanza mtu anayeteuliwa na rais hana maslahi yoyote kwa mwananchi badala yake ni kuwaingilia viongozi waliochaguliwa na wananchi kwa ajili ya kuvuruga amani na kushindwa kufanya kazi za maendeleo,” alisema Mbowe.


Alisema tatizo kubwa lipo kwa wakuu wa serikali kuruhusu kutumika na CCM ili kuleta chokochoko kwa mabaraza yanayoongozwa na CHADEMA, huku akitolea mfano mabaraza ya Hai, Arusha, Mwanza na Moshi ambapo kanuni zimekuwa zikivunjwa makusudi ili kusababisha madiwani waliochaguliwa na wananchi kushindwa kufanya kazi zao.


“Ukweli ni kwamba vikao vya halmashauri vipo kisheria na vinaweza kufanya maamuzi yake, lakini wakati mwingine vikao hivi vinaweza kuwa na madhaifu, hivyo ni vema mkuu wa mkoa na meya wakaitana mezani na kushauriana, kwani kuvutana kunakuwa hakuna mantiki yoyote.


“Kama ni matumizi mabaya ya fedha CCM imekwishafanya ubadhirifu mkubwa sana wa fedha ambao ulifanywa na viongozi tena wa chama hicho, najua huu ni mpango unaofanywa na CCM, lakini mimi Mbowe nasema CHADEMA itaendelea kujenga demokrasia ya haki kwa kuendelea kutamalaki kwa kupewa mamlaka na wananchi wenyewe, na siyo vinginevyo,” alisema Mbowe.


Mvutano uliopo kwenye Manispaa ya Moshi ni ule wa Mkuu wa Mkoa kuzuia safari ya madiwani, na watendaji kwenda Kigali Rwanda, safari ambayo ilikuwa igharimu sh milioni 123. Pia mkuu huyo alipingana na gharama hizo kwa kusema ni ndogo kwani itagharimu zaidi ya milioni 200.


Hata hivyo, Mbowe alisema kuwa kama madiwani wamekaa na kuona kuna umuhimu wa wao kufanya safari hiyo, ni vema mkuu wa mkoa angeheshimu maamuzi yao, kwani kama utaratibu huo ukiendelea madiwani waliochaguliwa na wananchi watashindwa kufanya maamuzi yao kwa kuongozwa na matamko kutoka kwa viongozi wa serikali.

uzi wa leo kutoka Jamii Forums

Wasira awakana watoto wake waliojiunga na chadema

Kutoka Gazeti la Mwananchi

Kashfa nyingine yaibuka Tanesco

KASHFA mpya imeibuka ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), baada ya kubainika kuwa vikombe vya kufungia nyaya za umeme vyenye thamani ya mamilioni ya fedha vimetelekezwa kutokana na baadhi ya vigogo wa shirika hilo kushindwa kunufaika na mradi huo.

Habari kutoka ndani ya shirika hilo zinaeleza kuwa vigogo hao wanadaiwa kuvikataa vikombe hivyo kwa maelezo kuwa ni vibovu, baada ya mzabuni kushindwa kuwaona vigogo hao.

Wakati vigogo hao wakivikataa vikombe hivyo kwa madai kuwa ni vibovu, taarifa zinaeleza kuwa wataalamu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wamethibitisha kuwa vikombe hivyo ni vizuri na havina matatizo yoyote.

Hatua ya Tanesco kupeleka vikombe hivyo kuthibitishwa na wataalamu wa Chuo Kikuu, Kitengo cha Uhandisi ilitokana na mvutano uliokuwapo baada ya vigogo walioshindwa kunufaika na mradi huo kutoa maelezo kuwa vikombe hivyo havina viwango bora.

Hata hivyo, uchunguzi unaonyesha kuwa licha ya vigogo hao kuvikataa vikombe hivyo zaidi ya 40,000 vyenye thamani ya Sh900 milioni kwa madai kuwa vibovu, tayari shirika hilo limekuwa likivitumia katika nguzo zake zenye umeme mkubwa kwa miaka mingi.

Familia ya Waziri Wasira yahamia Chadema

Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbroad Slaa akiwakabidhi kadi za uanachama wa CHADEMA watoto wa Wasira
 
Yadai inahitaji mabadiliko ya kweli
Yasisitiza udugu utabaki pale pale
WATOTO wa kaka yake Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Uhusiano na Uratibu, Steven Wassira wametangaza kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Kwa mujibu wa watoto hao, uamuzi wao wa kujiunga CHADEMA unatokana na kuona nuru ya mabadiliko kupitia chama hicho.

Vijana hao, Esther Wassira na Lilian Wassira ambao ni watoto wa George Wassira, walijiunga na chama hicho jana.

Walipokewa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbrod Slaa katika ofisi za makao makuu ya chama hicho Dar es Salaam.

Vijana hao ambao ni wanasheria, wamaliki Kampuni ya Uwakili ya Armicus Atorneys.

“Tuna haki ya kuchagua chama cha kujiunga nacho,Wassira ni baba yetu mdogo na atabaki kuwa hivyo lakini sisi tuna hiari ya kufanya kile tunachokiamini,”alisema Esther.

Esther ambaye ni mdogo wa Lilian, alisema hivi sasa Tanzania inahitaji mabadiliko ya dhati kwa kuunga mkono Vuguvugu la Mabadiliko (M4C kuondoa kero zinazokwamisha maendeleo nchini kwa zaidi ya miaka 50 sasa.

“Kwa mara ya kwanza nimeamua kujiunga na M4C, naiona CHADEMA ni chachu ya mabadiliko. Ni wakati mpya kukiweka chama hiki kwenye uso mwingine wa siasa.

“...huu ni mfumo wa vyama vingi, hatuwezi kuendelea na CCM ambayo siku zote inacheza ‘muziki’ na kufuata nyayo za Chadema. Bila shaka ni chama chenye sera nzuri.

“Sisi kama vijana tunaona bado tunayo nafasi ya kufanya kitu kupitia Chadema, lazima nifanye kitu kwa ajili ya nchi yangu naamini wanaweza kutufikisha pale tunapotaka,” alisema Esther.

Naye Lilian alitoa wito kwa Watanzania kuamini mabadiliko ya maendeleo yanawezekana kupitia chama hicho.

“Naamini hatujapotea, tuko sahihi na tumeingia chama sahihi, tunaona wanavyopambana, tumeamua kuwa sehemu ya mabadiliko… sifuati ukongwe wa chama bali sera zenye matumaini ya dhati kwa ajili ya kizazi chetu Watanzania.

“Tukiunganisha nguvu Tanzania mpya inakuja, bila madadiliko hakuna ushindani. Tunataka maendeleo, tumechoshwa na sera za CCM, naamini kwa msaada wa Mungu inawezekana,” alisema Lilian.

Akizungumza baada ya kuwapokea, Dk. Slaa alisema hatua yao hiyo ni kielelezo tosha kwamba yale yanayozungumzwa na CCM kupitia kwa Wassira kuwa Chadema ni chama cha vurugu na fujo ni propaganda zilizopitwa na wakati.

“Siamini watu wenye akili timamu kama vijana hawa wanaweza kujiunga na chama ambacho ni cha fujo na vurugu kama ambavyo imekuwa ikisema kwa nguvu kubwa na kupitia kwa Wassira,”alisema Dk.Slaa.

Kuhusu chama hicho kudaiwa kuwafanyia vurugu wafuasi wa Chama cha Wananchi (CUF) mkoani Arusha, Dk.Slaa alisema si haki kukihusisha chama hicho na vurugu hizo kwa sababu hakina hatimiliki na Arusha.

Alisema si kila mfanyabiashara ndogo ndogo (machinga) ni mwana Chadema.

“Kumezuka na upotoshaji kujenga dhana kwamba kila machinga wa Arusha ni mfuasi wa CHADEMA. Sisi hatuna hatimiliki Arusha, kila chama kinayo haki ya kufika kila kona ya nchi hii kufanya siasa bila kuingiliwa, lakini wasituhusishe na vurugu za CUF,” alisema Dk.Slaa

Mkutano wa Zitto Kabwe Karatu Mjini





Mdee Afungua Shina La CHADEMA Boko




Mdee `amshukia` Mchungaji Lwakatare

Serikali imetakiwa kumdhibiti na kumuondoa, kisha kuibomoa nyumba ya Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mchungaji Getrude Lwakatare.
Rai hiyo imetolewa na Waziri Kivuli, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee.
Taarifa kwa vyombo vya habari jana ilieleza kuwa, wakati raia wengine wakibomolewa nyumba ambazo kama ilivyo ya Mchungaji Lwakatare, zilijengwa kinyume cha sheria, Mbunge huyo amehamia na kuishi kwenye nyumba yake.
Julai mwaka huu, nyumba za wananchi waliojenga katika maeneo tengefu ya ufukwe wa Jangwani, mto Ndumbwi na mto Mbezi, zilibomolewa katika operesheni iliyoendeshwa na Baraza la Mazingira la Taifa (Nemc).
Operesheni ambayo ilihusisha takriban nyumba 15 na kuta nane. Lakini nyumba ya Mchungaji Lwakatare haikuguswa.
Hata hivyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk Terezya Huvisa, aliwahi kuwaambia waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa, nyumba hiyo haikubomolewa kutokana na pingamizi la mahakama.
Nyumba inayotajwa kuwa mali ya Mchungaji Lwakatare, imejengwa kwenye viwanja namba 2019-2020 Kawe Beach, katika fukwe za bahari ya Hindi.
Viwanja hivyo vinadaiwa kupatikana kwa ushirikiano wa Mchungaji Lwakatare na Frank Mushi.
Mdee alisema wakati kigogo huyo (Lwakatare) amehamia kwenye nyumba yake kwa matangazo na mbwembwe, mto Ndumbwi, bahari na mazingira kwa ujumla yameharibiwa, lakini zaidi kuwepo raia waliobomolewa kwa mujibu wa sheria hizo.
Mdee alinukuu Sheria ya Mazingira, sura 191 ya mwaka 2004, fungu 57(1), inasema hairuhusiwi kufanya shughuli zozote za kudumu za kibinadamu ndani ya mita 60.
Mita hizi ni ambazo kwa asili yake zinaweza kuhatarisha au kuathiri ulinzi na utunzaji wa mazingira, utunzaji wa bahari, kingo za mto, bwawa au mwambao wa asili wa ziwa.
Sheria nyingine ni ya ardhi, namba 4 ya mwaka 1999, sura 113, fungu la 7 (1) (d), ikieleza kwamba eneo lolote lililo ndani ya mita 60 kutoka kingo ya mto na bahari, linatakiwa kutangazwa kama ardhi hatari au kuhifadhiwa.
Na pale inapotokea kuwa masharti ya sheria moja yanapingana na masharti ya Sheria ya Mazingira, kuhusu mambo yanayohusu usimamizi wa mazingira, sheria hiyo inatumika, kwa mujibu wa fungu 232 la sheria ya mazingira sura 191 ya mwaka 2004.
”Kutokana na hali hii, serikali inatakiwa kujinasua katika mwendelezo wa tafsiri wanayoipata wananchi kuwa imetekwa na kuwekwa mfukoni na watu wachache wenye uwezo,” alisema.
Aliongeza,” maana wanaona kuwa huu ni mwendelezo wa serikali kuwa na kigugumizi pale sheria zinapovunjwa na vigogo serikalini, au watu wenye fedha wanaoshirikiana na baadhi ya viongozi wa serikali na chama tawala kufanya ufisadi.”
Alisema hali ilivyo sahihi inadhihirika kuwepo kundi la wanaojiona wapo juu ya sheria, huku wanyonge wakishughulikiwa.
”Ni wakati kwa mawaziri wanaohusika na masuala ya ardhi na mazingira kuwaeleza Watanzania kulikoni wananchi wa hali ya chini kuvunjiwa nyumba wakati Mchungaji Lwakatare, ambaye uharibifu wake ni wa hatari kuliko waliovunjiwa akitamba mtaani, ” alidai.
Mdee alitafsiri kitendo hicho kama ni Mchungaji Lwakatare kutamba kuwa yuko juu ya sheria na hakuna mamlaka yoyote yenye uwezo wa kumzuia kufanya alichofanya.
”Ni aibu kwa Taifa kuwa na viongozi wa aina hii! Viongozi ambao wako tayari kutumia fedha, hila, mamlaka na dhamana za uongozi walizopewa, kuhalalisha haramu, ni janga kwa mstakabali wa taifa letu,” alisema.
Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Terezya Huvisa, hawakupatikana kuelezea juu ya tamko la Mdee.
Mawaziri hao walikaririwa kwa nyakati tofauti wakisema nyumba zote zilizojengwa kando kando ya fukwe za bahari na mito zitabomolewa

TAMKO LA CHAMA KUKANUSHA SHUTUMA ZA CHAMA CHA CUF KUFANYIWA VURUGU NA CHADEMA.

TAMKO LA CHAMA KUKANUSHA SHUTUMA ZA CHAMA CHA CUF KUFANYIWA VURUGU NA CHADEMA.
Ndugu wananchi na wanahabari,

Siku ya terehe 27 Alhamisi Septemba 2012 chama cha wananchi CUF walitoa taarifa ya malalamiko kwa vyombo vya habari na mitandao kuwa wanachama wa CHADEMA wamewafanyia vurugu kwa kuwapiga mawe na kuwa jambo hilo limehamasishwa na viongozi wa chama katika mkoa wa Arusha pamoja na Mhe Godbless Lema.
Wote tunafahamu kuwa siku hiyo hiyo katika viwanja vya soko la Kilombero wafanyabiashara ndogo ndogo walikuwa wamevamia na walikuwa wakijigawia maeneo, baada ya eneo la awali walilopewa la viwanja vya NMC kushindwa kuwachukua wafanyabiashara wote na halmashauri kushindwa kutoa majibu kwa wafanyabiashara hawa ambao waliwaambia wote waende NMC.
Kwanza tunapenda kutoa pole kwa viongozi wa CUF kwa jambo hili lililowapata. Wao kama watu na Watanzania wenzetu tunawapa pole sana.
Pili, CHADEMA inakanusha kuhusika na jambo hili. Hii si tabia ya CHADEMA na kamwe haiwezi kuwa tabia ya CHADEMA kufanya siasa chafu za namna hiyo. CHADEMA tunajali sana amani na upendo, na hii ndiyo tabia na makuzi yetu Watanzania.
Katika mazingira haya, CHADEMA tunachukua fursa hii kuvikaribisha vyama vyote mathalani CUF, Arusha ni yetu sote na tutumie demokrasia vizuri kufanya kazi nzuri ya siasa kwa ajili ya kusababisha na kuleta matumaini kwa Watanzania hawa ambao serikali ya chama cha mapinduzi imeshindwa kuwaletea.
CHADEMA hatuna shida na ushindani wa kisiasa katika mazingira ya kidemokrasia kwa maana ndio wakati pia wa wananchi kupima na kujua nani mkweli na ama nani anafanya kwa dhati ya kweli. Hivyo tunawakaribisha CUF karibuni Arusha na wala wasitafute kisingizio cha kuegemea ili CUF ianze kutajwa tajwa kwa kutumia mgongo wetu.
Sambamba na hili, CHADEMA mkoa wa Arusha tumesikitishwa sana na tamko la CUF lilitolewa na Naibu Mkurugenzi wa Habari, Uenezi na haki za BInadamu Mhe Abdul Kambaya, tamko lenye matisho na lugha isiyofaa. Moja na maneno ya tamko hilo wamesema, nukuu “Uwezo wa kuwafanya tutakavyo tunao na kwa sababu wameanza tunaweza kumaliza”. Wakazi wa Arusha na Watanzania wapime na waone, haya si maneno yanayoweza kutoka kwenye kichwa cha mtu anayefikiri vizuri, mtu anayeipenda nchi yake na kuheshimu utawala wa sheria. Zaidi ya hapo tamko hilo limesema pia, “Ile ngangari kwa polisi tunaweza kuwahamishia wao wakose pa kukaa”.
Katika yote haya, niwaombe wakazi wa Arusha, Wanachadema na hata wanachama wa vyama vingine tuwapende na tuwakaribishe CUF Arusha na sote tufanye kazi ya siasa kwa nguvu za hoja. CUF wanaweza kufanya hicho wanachotaka kufanya lakini CHADEMA kamwe hatupo tayari kwa vurugu ya aina yoyote, aidha tunawakaribisha kwa moyo mmoja na kama wapo tayari basi tufanye siasa zenye tija na manufaa kwa wakazi wa Arusha.
Aidha nitoe onyo kali sana kwa mamluki ambao wamekuwa wakijifanya kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu. Mara kadhaa watu hawa wamekuwa wakisababisha fujo ili kukifanya CHADEMA kionekane kuwa ni chama cha vurugu. MAMLUKI ni sumu, tukimgundua na kumthibitisha mtu wa aina hiyo katikati yetu tutamtangaza mbele ya jamii kuwa yeye ni sumu na kuomba wananchi wamtenge maana anapingana kwa kuleta hila na unafiki kwenye kazi ya kuwakomboa Watanzania. Niwatangazie mamluki hamtatuweza na tutawagundua tu.
Mwisho, tunapoelekea kwenye marudio ya uchaguzi mdogo kwenye kata za Daraja II kwa Arusha mjini na Bangata kwa wilaya ya Arumeru Magharibi, nirudie kusema maneno ya Mhe Lema kuwa iwapo viongozi na watumishi wa umma watajihusisha na kushiriki kwa kufanya kampeni za kisiasa wakiwa wanatumia magari na vifaa vingine vya serikali watu hawa tutawakamata na tutawapeleka huko wanakostahili kupelekwa wezi na vibaka wengine. Hii ni tahadhari tunamaanisha kweli na wananchi wote wawe makini “wakamate mwizi” lengo likiwa ni kuweka adabu kwa watumishi na viongozi umma wanaovunja sheria ya utumishi wao kwa umma na matumizi ya rasilimali kwa namna isivyotakiwa kisheria. CHADEMA tutashiriki chaguzi hizi na tunawaomba wakazi wote wa maeneo haya tushiriki kwa utulivu na amani.
WANACHADEMA wote tuendelee kuwa majasiri, tusiwe waoga na tusimamie kweli na haki.
“Hakuna kulala Mpaka Kieleweke”
Amani Sam Golugwa
KATIBU WA CHADEMA MKOA WA ARUSHA: golugwa@gmail.com

John Heche afichua mbinu chafu zinazoelekezwa kwa Chadema


 
Mpango wa kusitisha M4C, baada ya ccm kugundua kwamba mbinu zote za kusitisha M4C kwa kutumia polisi na dola zimegundulika baada ya kujaribu kutumia vifo vya Morogoro na Iringa kushindikana sasa wameamua kuwatumia CUF, mpango unaonyesha kwamba CUF watakwenda kwenye maeneo ambayo chadema ina nguvu kubwa sana kama Arusha, Mbeya, Mwanza, Manyara, Kiliman jaro,morogoro, Shinyanga,Mara na maeneo mengineyo
 
 

Mbali na hilo watafanya mikutano ambayo itakua na lugha za matusi na kejeli na kuikashfu Chadema na viongozi wake ili wapenzi na wanachama wa chadema wawafanyie fujo hao wanaotukana au watumie watu watakaovalishwa nguo za chadema kuanzisha fujo kwenye mikutano ya CUF ili ionekane kwamba CUF wanafanyiwa fujo baada ya kuoneka hivyo Cuf watawataka wanachama wao pia kuifanyia chadema fujo na hivyo serikali itaingilia kati kufuta operesheni M4C na kile kilichoanzishwa na CUF kwa jina la V4C na malengo ya ccm kutuzuia kwenda vijijini kuwaamshaWatanzania yatatimia kwa kutumia justification kwamba mikutano hiyo inafujo kwahiyo imefutwa au kusitishwa na hapo CUF watakubali kwa haraka maana ni mpango wa pamoja, nachukua fursa hii kuwaomba vijana wa Chadema popote walipo wasifanye fujo au hata kutukana mtu hata wakifanyiwa fujo wasijibu maana tutawapa fursa wabaya wetu kutumaliza, tunaikaribisha sana CUF popote ili wajipime na kuona je ni washindani wetu kweli? sisi hatushindani na CUF wala chama kingine chochote cha upinzani bali adui yetu ni ccm, ninawaomba viongozi wa vyama vya upinzani hasa Cuf kuacha kutumiwa na dola kufifisha harakati za watanzania kuleta mabadiliko ya kweli katika nchi hii kwa kutumia chama chao cha demokrasia na maendeleo chadema.

MUNGU IBARIKI CHADEMA, MUNGU IBARIKI TANZANIA, HAKUNA KULALA MPAKA KILEWEKE

Tuesday 25 September 2012

CHADEMA: Kama safari ya kifisadi RC atushitaki

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Manispaa ya Moshi kimemtaka Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama, kutumia vyombo vya ulinzi na usalama kuwakamata na kuwashitaki madiwani kwa kile anachodai ufisadi uliotaka kufanywa na madiwani hao katika safari yao ya mafunzo Kigali nchini Rwanda.
CHADEMA kupitia makada wake maarufu, James ole Millya na Jafary Michael walitoa kauli hiyo kwa nyakati tofauti wakati wa mikutano ya hadhara iliyoanza hivi karibuni katika maeneo mbalimbali ya mji wa Moshi kutoa ufafanuzi kwa wananchi wa hatua ya mkuu huyo wa mkoa kuzuia safari hiyo huku wakiita ni ya kisiasa zaidi.

Mapema mwezi huu, Gama aliwaambia waandishi wa habari mbele ya kamati ya ulinzi ya mkoa kuwa amesitisha safari hiyo ambayo ingegharimu sh milioni 123.2.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Penford vilivyoko katikati ya mji wa Moshi, Meya wa manispaa hiyo, Jafary Ally, alisema fisadi yeyote anapothibitika anachukuliwa hatua za kisheria.

“Ndugu zangu wananchi wa Moshi, kama kweli Gama anaona kile madiwani wa CHADEMA walichotaka kukifanya ni ufisadi….. leo hii hakuna hata mmoja wetu ambaye angekuwa katika eneo hili la mkutano, wote tungekuwa gerezani.

Alisema mkuu huyo wa mkoa sasa ameacha majukumu yake ya kiserikali na kuanza kutumika kisiasa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa lengo la kuwagombanisha madiwani hao ambao wengi wao wanatoka CHADEMA.

Meya Michael alisema fedha zilizotengwa kwa ajili ya kuwajengea uwezo madiwani zitatumika kama zilivyopangwa na kama mkuu huyo wa mkoa akiendelea kutumika kisiasa na kuacha shughuli za utendaji wa kuwatumikia wananchi, watatangaza mgogoro naye wa kutoshirikiana kwenye shughuli zozote.

Tanzania Daima

CHADEMA kuzindua matawi kila kata

 
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinatarajia kuzindua matawi katika kila kata nchini, ili kujihakikishia ushindi wa asilimia kubwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwaka 2014 nchi nzima.

Kauli hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika, katika ziara ya ufunguzi wa matawi na msingi 10 ya chama hicho kata ya Kimara.

Akizindua tawi la Kilungule ‘B’, Mnyika aliwaambia viongozi wa matawi hayo kuziona ofisi hizo kama mbadala wa ofisi za Serikali za Mtaa zinazoongozwa na CCM kwa kuwasaidia wananchi.

Aliwataka viongozi hao kutumia changamoto na matatizo wanayopelekewa na wananchi kuwabana wenyeviti wa serikali za mitaa, ili kuhakikisha hawarudi mwaka 2014.

“Ndugu zangu wa Kilungule ‘B’ pamoja na changamoto za kisiasa mlizokuwa nazo mmefanikiwa kujenga ofisi za matawi na misingi … zitumieni vizuri, ili tuweze kupata ushindi mkubwa katika chaguzi zinazokuja,” alisema.

Mnyika pia amewakabidhi viongozi wa matawi hayo taarifa za mipango na matumizi ya maendeleo ya jimbo lao ili kuhakikisha wanafuatilia kwa karibu mambo yanayotekelezwa na yasiyotekelezwa na serikali.

pamoja na mambo mengine, Mnyika alitumia fursa hiyo kutoa mwongozo wa kudai Katiba mpya, ili kuhakikisha mwaka 2015 wanapata Katiba itakayowaondolea dhuluma nyakati za uchaguzi mkuu.

Tanzania Daima

Thursday 20 September 2012

Jaji Mkuu, Othman Chande aahirisha kesi ya rufaa ya Godbless Lema

Jaji Mkuu wa Tanzania, Othman Chande ameahirisha kesi ya rufaa ya aliyekuwa mbunge wa Arusha Mjini, hadi Oktoba 2, 2012 kwa mujibu wa maombi ya mawakili wa pande zote mbili, CCM na CHADEMA walioandika barua ya kuomba kuahirishwa kwa kesi hiyo baada ya kifo cha mzazi wao ambaye maziko yake yanatarajiwa kufanyika Septemba 22, 2012.

Jaji Mkuu ametoa amri fupi ya Mahakama kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye alikuwa anajibu maombi wa pili aunganishwe kama mtu muhimu katika kesi hiyo.

Kesi hiyo ambayo imesikilizwa kwa takribani saa mbili chini ya Jaji Mkuu na Majaji wengine wawili wa Rufani, ni ya kukata rufaa kupinga kuvuliwa ubunge wa aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA).

Mara baada ya kesi hiyo kuhairishwa, umati mkubwa uliokuwepo mahakamani hapo uliondoka hadi katika ofisi za CHADEMA ambapo Lema aliongea na wananchi waliokuwa wakimsindikiza na kuwasihi kuwaombea Majaji wa kesi hiyo ili waweze kutoa hukumu ya haki, “mimi sio kwamba nataka nishinde na wala siogopi kushidwa ila naomba tuwaombe hawa majaji wa kesi hii ili waweze kutoa maamuzi ya haki yasiyomgandamiza mtu yeyote,na napenda pia kuchukuwa nafasi hi kuwaeleza kuwa jumanne tunatarajia kufanya mkutano katika kiwanja cha ngarenaro ambapo hapo ndipo tutakapo fungua kampeni zetu za udiwani rasmi,” alisema Lema.

Katika kesi hiyo, Lema anatetewa na Tundu Lissu, wakati kaka yake, Alute Mughwai, anawatetea walalamikaji.

Wakili Mughwai anashirikiana na wakili Modest Akida kuwawakilisha wadaiwa kwenye shauri hilo ambao ni wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo, waliofungua shauri lililotengua ubunge wa Lema wakidai kuwa wakati wa kampeni alimdhalilisha mgombea wa CCM, Dkt. Batilda Burian kwa kutumia lugha za matusi.

Awali, Lema kupitia wakili wake, Method Kimomogoro, anayesaidiana na Lissu, aliwasilisha kwenye mahakama hiyo hoja 18 za madai akipinga kutenguliwa kwa ubunge wake na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Aprili 5, mwaka huu.

Kwenye baadhi ya madai hayo, Lema aliiomba Mahakama ya Rufaa kutengua uamuzi wa Mahakama Kuu, uliotengua ubunge wake, huku akiitaka imtangaze kuwa mbunge halali wa Jimbo la Arusha Mjini.

Aidha, aliitaka mahakama hiyo ya juu, iwaamuru walalamikiwa katika shauri hilo walipe gharama za rufaa hiyo pamoja na zile za kesi iliyomalizika kwenye Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.

Katika madai mengine, Lema anamlalamikia Jaji Gabriel Rwakibarila, aliyesikiliza kesi hiyo kuwa alitoa uamuzi wake kwa kuzingatia maneno ya uvumi, huku akipuuza ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.

Lema anadai kuwa jaji alikosea wakati alipoamua kuwa mpiga kura yeyote anaruhusiwa kupinga matokeo ya uchaguzi hata kama haki zake za msingi hazijaguswa.
 
 
 
 
 
Kamanda lema akiwa nje ya mahakama

Kamanda Lema wakati anaingia Mahakamani leo

Wananchi wa Arusha mjini wakimsikiliza Kamanda Lema kabla ya kwenda mahakamani leo.
 
 
 
 
 
 
 
 

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU